Header Ads

test

IRENE UWOYA ADAI HAVUTIWI NA WANAUME WENYE MIONEKANO MIZURI


Iko wazi, katika ile list ya wasichana warembo kutoka kwenye kiwanda cha Bongo Movie huwezi kusahau kumtaja Irene Uwoya, hii ni kutokana na yeye alivyojiweka kwenye suala zima la urembo wake au uzuri wake na kumfanya kutoshuka wala kupanda.

Muigizaji huyo ambaye ameandaa event maalum kwaajili ya Valentine’s Day aliyoipa jina, ‘Irene Uwoya Valentine’s Special Night, ameahidi kueleza baadhi ya mambo ambayo watu hawafahamu kuhusu yeye katika sekta ya malavidavi. Leo Feb 8, Irene kanyoosha maelezo juu ya kile anachokiamini hasa katika suala zima la mahusiano.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, ameandika.. “Kitu ambacho hamkijui kuhusu mimi ni kuwa SIJAWAHI kuvutiwa na wanaume wenye mionekano mizuri, sielewi ni kwanini lakini wanaume wenye sura mbaya huwa wanaamsha hisia zangu za KIMAPENZI”

Kuelekea siku ya Valentine, kwa mujibu wa muigizaji huyo atakuwa akitoa fact moja moja kila siku ambazo tulikua hatuzijui kutoka kwake, na kwa fact hii ya kwanza inaweza kuamsha ari kwa wanaume waliokua wanaamini wana mionekano isio mizuri nao kujiona wako kwenye kundi la kupendwa na warembo.

No comments