Header Ads

test

IEBC: Mfumo wetu wa matokeo haukudukuliwa


Tume ya uchaguzi nchini Kenya imesema kuwa mfumo wake wa kutoa matokeo haukudukuliwa kama ilivyodaiwa na upinzani.
Mkurugenzi mkuu wa tume hiyo Ezra Chiloba amesema kuwa madaia yaliotolkewa na mgombea wa upinzani Raila Odinga hayana msingi wowote.
Amesema kuwa tume hiyo imefanya uchunguzi kubaini hayo.
Ameongezea kuwa kufikia sasa wamepokea fomu 29,000 34A na kwamba wanatarajia fomu zote 40,000 kufikia kesho alfajiri.
Vilevile ameongezea kuwa upigaji kura umkamilika katika vituo vyote nchini

Matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais kufikia sasa

Katika matokeo ya awali ya vituo 39620 out of 40883 yaliyopakiwa na IEBC mtandaoni:
  • Uhuru Kenyatta wa Jubilee ana kura 8009175 votes (54.31%)
  • Raila Odinga wa ODM ana kura 6608405 votes (44.81%)
Kura zilizoharibika kufikia sasa ni 393969

No comments